Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete akifungua jengo la hazina ya Benki kuu ya Tanzania tawi la Dodoma
RAIS Jakaya Kikwete amesema kumekuwa na nidhamu kwenye matumizi ya fedha za serikali pamoja na kuongezeka kwa mapato yake. Alisema hayo jana mjini hapa wakati akifungua majengo ya Hazina,
Benki Kuu tawi la Dodoma na Ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali.
Rais Kikwete alisema tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), mapato ya fedha za serikali yameongezeka. “Kumekuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha na ukusanyaji wa mapato
umeongezeka,” alisema Rais Kikwete na kuongeza kuwa miongoni mwa mambo
yaliyochangia kuongezeka kwa ufanisi ni pale serikali ilipoajiri
wahasibu ngazi ya CPA wapatao 780 kwenye halmashauri za wilaya ambako
awali hata uandishi wa vitabu vya hesabu ulikuwa ni tatizo. “Tumefika
mahali pazuri, taarifa nzuri na makosa mengi yamerekebishwa,” alisema na
kuongeza kuwa pia ofisi nyingi za ukaguzi ziko kwenye majengo ya
serikali, jambo linalofanya wakaguzi wasiwe huru kufanya kazi zao.
Alisema ameridhishwa na viwango vya ubora wa majengo yaliyozinduliwa
na kutaka kuboreshwa kwa eneo linalozunguka majengo hayo ili yaendelee
kuwa na hadhi yake.
Alisema sehemu ya mbele ya majengo kukiwa kuchafu thamani ya majengo
inashuka, hivyo itengenezwe bustani ili majengo yawe na thamani. “Nimemwambia Mkuu wa Mkoa hatutegemei kati ya majengo haya wananchi
wagawiwe viwanja lazima kupanda miti vizuri kulia na kushoto na viwanja
vinavyogawiwa kuwe na viwango vya majengo,” alisema Rais Kikwete.
“Pangeni mji vizuri ili Dodoma ipendeze polepole hii ndio safari ya
kujenga makao makuu,” alisema Rais Kikwete na kuagiza kupimwa kwa eneo
lote la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ili kusiwe na mji hohela.
Awali, Waziri wa Fedha, Saada Mkuya alisema ujenzi wa majengo hayo ni
utekelezaji wa maagizo ya serikali kujenga na kuendeleza makao makuu ya
serikali Dodoma.
Ujenzi ulianza mwaka 2010 kwa ujenzi wa jengo la (BoT), jengo la
Hazina na mwaka 2012 ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mdhibiti Mkuu wa Hesabu
za Serikali.
Sign up here with your email