Mgombea Ubunge Kupitia Chadema Jimbo la
Mbinga Magharibi ndugu Cuthbert Ngwata amepata ajali mbaya ya gari usiku
alipokuwa akielekea kwenye kampeni ya Ubunge. Kulingana na Mtoa taarifa
Mgombea Ubunge huyo wa Chadema alipata ajali baada ya gari yao
waliyokuwa wanasafiria kuvamiwa na watu waliokuwa wanataka kuwateka
ndipo dereva wa gari hilo katika harakati za kuwakimbia ndipo gari
likayumba na kuingia Korongoni na kusababisha ajali hiyo mbaya.
Kulingana na mtoa taarifa ndani ya gari hiyo kulikuwa na mtu mwingine
anayejulikana kama kamanda Pompi anayetokea Mbozi Mkoani Mbeya ambaye
amefariki dunia katika ajali hiyo.
Awali mgombea ubunge huyo ndugu Cuthbert Ngwata pamoja na dereva wake walikimbiziwa katika hospitali ya Nyasa kwa matibabu lakini kutokana na hali zao kuwa mbaya sana wamehamishiwa kwenye hospitali ya Litembo kwa matibabu zaidi.
Awali mgombea ubunge huyo ndugu Cuthbert Ngwata pamoja na dereva wake walikimbiziwa katika hospitali ya Nyasa kwa matibabu lakini kutokana na hali zao kuwa mbaya sana wamehamishiwa kwenye hospitali ya Litembo kwa matibabu zaidi.
Hili
ni tukio la pili kuwapata wagombea Ubunge wa Chadema katika kipindi
kisichopungua wiki tatu. Ikumbukwe tukio kama hili liligharimu maisha ya
mgombea Ubunge wa Lushoto ndugu Mohamed Mtoi wiki chache zilizopita.
Mpaka sasa hakuna taarifa rasmi zinazoelezea mazingira ya kifo
kilichompata Ndugu Mohamed Mtoi.
Kutokana na mfululizo wa matukio haya tunaliomba jeshi la Polisi lifanye Uchunguzi kujua namna gani kumekuwa na matukio kama haya yanayowapata wagombea Ubunge katika kipindi hiki cha kampeni. Pia wagombea Ubunge wote wachukue Tahadhari za kiusalama wanapokuwa katika harakati za kampeni kwa kuepuka kutembea safari za Usiku wanapokuwa katika kampeni, na pia kuwa na Ulinzi wa kutosha ili kuepuka matukio kama haya kuwakumba
Kutokana na mfululizo wa matukio haya tunaliomba jeshi la Polisi lifanye Uchunguzi kujua namna gani kumekuwa na matukio kama haya yanayowapata wagombea Ubunge katika kipindi hiki cha kampeni. Pia wagombea Ubunge wote wachukue Tahadhari za kiusalama wanapokuwa katika harakati za kampeni kwa kuepuka kutembea safari za Usiku wanapokuwa katika kampeni, na pia kuwa na Ulinzi wa kutosha ili kuepuka matukio kama haya kuwakumba
Source: http://chademablog.blogspot.com/
Sign up here with your email