Kingunge ajitoa rasmi CCM leo


Mwanasiasa Mkongwe Mheshimiwa Kingunge Ngombare Mwiru leo ametangaza kujiondoa ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM na sasa atakuwa mwananchi huru.

Kingunge amezungumza leo mbele ya waandishi wa Habari akiwa nyumbani kwake Kijitonyama, Dar es salaam. Amesema kutokana na matukio yaliyotokea katika kumpata mgombea Urais kupitia chama chake ni tofauti na ilivyokuwa mwaka 1995 na 2005 hivyo ameamua kuondoka ndani ya chama hicho na sasa yupo huru.
Kingunge amesema ameamua kufanya hivyo kutokana na kile alichoamini kuwa CCM haifanyi yale yaliyoasisiwa na kujengewa Misingi bora na waasisi wake. Aidha amesema hakusudii kujiunga na Chama Chochote cha Siasa nchini bali atakuwa mtanzania huru.

Kingune amesema hawezi kuhimili chama kisichojiendesha bila katiba na anajua uamuzi wake utawasumbua baadhi ya ndugu zake, wazee na makada wengine. Mwanasiasa huyo amesema kwa sasa hakusudii kujiunga na chama kingine chochote kwa kuwa amekuwa mwanaharakati kwa miaka 61.
Pia amesema yeye ni raia na ana haki zake za kisiasa na kijamii na ataendelea kuwa na mahusiano mazuri na nchi yake.Hali ya sasa jinsi ninavyoona vijana, wafanyakazi, wakulima wanataka mabadiliko na mimi nipo upande wa mabadiliko kwa sababu wakati tukiwa TANU tulifanya mabadiliko na kuunda CCMKINGUNGE

Akizungumzia hali ya sasa kisiasa amesema kila kipindi katika jamii ya kitanzania hivi sasa inataka mabadiliko. Kingunge ametangaza uamuzi wake huo hivi pinde katika mkutano wake na waandishi wa habari ambao unarushwa moja kwa moja na kituo cha Televisheni cha ITV. 
Previous
Next Post »
Show Comments: OR

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com