Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa uzalishaji wa umeme wa maji kwenye mabwawa hayo umeshuka hadi kufikia megawati 105 kutoka 561 kutokana na ukame unaoendelea majira haya ya kiangazi.
Mramba alisema hali hiyo imeilazimu Tanesco kutegemea kwa kiasi kikubwa umeme unaozalishwa na mitambo ya mafuta na gesi asilia hasa ile ya Kinyerezi I, ili kupunguza makali ya mgawo huo kwa kuwasha mtambo mmoja baada ya mwingine hadi mwishoni mwa Oktoba.
Mramba alisema mgawo huo pia unatokana na kushuka kwa kiwango cha uzalishaji gesi ya ya Songo Songo, ambako Kampuni ya Pan Africa inafanya ukarabati wa visima baada ya kubaini uzalishaji ulikuwa ukishuka kutoka megawati 340 hadi 260.
Hata hivyo, alisema neema itaanza kuonekana leo kwa wakazi wa Dar es Salaam ambao huenda makali ya mgawo wa umeme yakapungua baada ya mtambo mpya wa megawati 35 kuwashwa jana kwa kutumia bomba jipya la gesi.
“Wananchi wawe watulivu mgawo huu hauna siasa hata chembe bali ni masuala ya kiufundi tu,” alisema Mramba.
Sign up here with your email