MERU: GARI YA TUME YA UCHAGUZI YANUSURIKA KUCHOMWA MOTO


Wananchi wa Kata ya Embaseni wilaya ya Meru jana walifanya fujo na kutaka kuchoma gari la Utalii ambalo limekodishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa Halmashauri ya wilaya ya Meru kwa madai ya kuwa lilibeba kura hewa na kutaka kuziingiza vituoni.

Hali hiyo imetokea jana katika kata hiyo majira ya saa 3:30 asubuhi hadi saa 4:00 asubuhi mara baada ya vijana kulisimamisha gari hilo kwa muda na kudai kuwa limebeba kura hewa na kutaka kulichoma moto.

Mara baada ya wasimamizi wa NEC waliokuwa ndani ya gari hilo kuwaeleza vijana hao kuwa gari hilo halina kura hewa bali lina fedha za kuwalipa wasimamizi wa uchaguzi na kila kata magari hayo yapo lakini halina kura hewa.
“Hakuna kura hewa na wala hatuna mpango wa kuiba kura bali hili gari limebeba fedha za kuwalipa wasimamizi wa uchaguzi na kama mnataka tuwaonyeshe majina yao ili mthibitishe na kiwango cha fedha wanachostahili kulipwa,” alisema.

Mara baada ya purukushani hiyo askari waliokuwepo eneo la tukio waliwaamuru vijana hao kuondoka na kwa wale wanaosubiri kupiga kura wapige kura kwani hakuna kura yoyote iliyobebwa ndani ya gari hilo.

Msimamizi wa Uchaguzi Wilaya , Jimbo la Arumeru Mashariki, Damari Mchome alisema kuwa si kweli kama watu wanavyodai kuwa gari hilo lilibeba kura hewa bali ukweli ni kuwa gari hilo lilibeba fedha kwa ajili kuwalipa wasimamizi wa NEC waliochaguliwa na halmashauri hiyo.

Alisema pia halmashauri hiyo imekodisha magari 26 kutoka kampuni mbalimbali za utalii kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi wa NEC kwani halmashauri hiyo ina magari matano tu ambayo hayatoshelezi kutoa huduma kwa Jimbo la Arumeru Mashariki.

Mchome alisema ndani ya gari hilo kulikuwa na mhasibu pamoja na msimamizi wa uchaguzi msaidizi pamoja na orodha ya malipo kwa wasimamizi wa NEC na gari hilo ambalo hakulitaja namba zake kuwa lilikuwa na kiasi cha zaidi ya Sh milioni sita ambazo baada ya tafrani hiyo fedha zipo salama na hakuna kura yoyote itakayoibwa.

Halmashauri hiyo ina jumla ya wapiga kura 160,647 na vituo vya wapiga kura vikiwa ni 437 na kata 26. Hata hivyo wananchi wa Jimbo la Arusha Mjini wanamchagua Rais na madiwani kutokana na Mgombea Ubunge wa ACT-Wazalendo Estomih Mallah kufariki dunia.





Chanzo: Habari leo
Previous
Next Post »
Show Comments: OR

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com