Halmashauri, Wilaya na Majiji yaagizwa kutenga bajeti ya kugharamia huduma za watu wenye Albinisim


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2015, Juma Khatib Chum,akizindua mradi wa kilimo cha umwangiliaji cha vitunguu kijiji cha Nkungi wilaya ya Mkalama.Chum aliagiza vijana waache kukaa vijiweni na badala yake waelekeze nguvu zao katika shughuli mbalimbali zitakazowapatia kipato ikiwemo kilimo cha umwangiliaji.


Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru 2015, Juma Khatib Chum, akikabidhi baadhi ya misaada ikiwemo simu za viganjani kwa walemavu wa ngozi (Albino) wa wilaya ya Mkalama.

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2015,Juma Khatib Chum,amezihimiza halmashauri za wilaya, manispaa na majiji nchini, kutenga bajeti kwa ajili ya kugharamia huduma za watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) kwa madai kwamba wengi wao hali zao kiuchumi ni duni.

Chum ametoa wito huo muda mfupi baada ya kukabidhi misaada mbalimbali ikiwemo kadi za kujiunga na mfuko wa afya ya jamii (CHF) kwa walemavu wa ngozi 28 wa wilaya ya Mkalama.Alisema watu wenye ualbino,wanayo mahitaji maalum mengi ikiwemo mafuta ya ngozi ambayo gharama yake ni kubwa,hivyo inakuwa ngumu kwao kumudu gharama hizo.


“Ili kulisaidia kundi hili dogo la watu wenye ualbino ambao wengi wao familia zao zina kipato duni,ni halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya kuwahudumia hawa ndugu zetu”alifafanua Chum.Aidha, kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru, amemtaka kila Mtanzania kuwa mlinzi kwa watu wenye ualbino,ili kuwalinda/kuwakinga na watu wenye lengo la kuwadhuru kutokana na imani zao potofu, kwa viungo vya walemavu hao,ni dili la kupatia utajiri.


Chum alitumia fursa hiyo kuishukuru na kuipongeza serikali ya wilaya Mkalama chini ya DC wake Fadhili Nkurlu kwa ubunifu wao wa kuwasaidia watu wenye ualbino. “Toka tumeanza kukimbiza mwenge wa uhuru mwaka huu na sasa tumebakiza mkoa moja tu tumalize mbio hizi,hatujaona mradi mzuri kama huu wa kuwahudumia ndugu zetu wenye ualbino”,alisema.
 
Alisema kitendo hiki ni kwamba mnajenga mazingira mazuri ambayo yatachangia ndugu zetu hawa, wajione kuwa na wao ni sehemu ya jamii  ya Watanzania. Awali mkuu wa wilaya ya Mkalama Nkurlu, (kwa sasa amehamishiwa wilaya ya Arusha) alitaja baadhi ya misaada waliyoitoa kwa walemavu hao wa ngozi,kuwa ni simu za viganjani na filimbi ambazo zitawasaidia kutoa taarifa juu ya usalama wao.
 
Alitaja mingine kuwa ni kadi ya mfuko wa afya ya jamii (CHF) ambayo watapatiwa matibabu kwa mwaka mzima bila ya kuongeza fedha yoyote,na pia wamepatiwa kofia za kujikinga na mionzi ya jua. “Katika juhudi za kuimarisha huduma kwa watu wenye ualbino, tunatarajia kufungua dirisha maalum kwenye vituo vya afya kwa ajili yao kupata matibabu bila usumbufu.Tutatenga bajeti katika mwaka wa fedha ujao na tunatarajia kuanzisha miradi mbalimbali kwa ajili ya Chama Cha Walemavu wa ngozi wilayani kwetu”,alisema Nkurlu.
 
Kwa upande wake mlemavu wa ngozi, Hidaya Omari,ametumia nafasi hiyo kuiomba serikali ihakikishe wataalam wa masuala ya ualibino,wanapatikana kwa karibu zaidi.Kitendo hicho kitasaidia kubaini mapema dalili za kansa ya ngozi.

Kwa mujibu wa Afisa mahusiano wa Chama Cha Walemavu wa ngozi Tanzania, Josephat Tona,watu wenye ualibino asilimia 80 ambao wengi wao wanaishi miaka 32,hufariki dunia majumbani kutokana na kukosa wataalam wa masuala ya walemavu hao.

Mkoa wa Singida wenye wilaya sita, una daktari moja tu ambaye hata hivyo hana usafiri wa kumwezesha kuwafikia walemavu wa aina mbalimbali wakiwemo na wa ngozi.

Chanzo: Dewjiblog 

Previous
Next Post »
Show Comments: OR

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com