Magufuli asema Shirika la Maendeleo ya Milenia (MCC) limemrahisishia kazi ya kusambaza Umeme

Dk. John Magufuli
 
MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli, amesema Shirika la Maendeleo ya Milenia (MCC), limemrahisishia kazi ya kutoa fedha kwa Tanzania ya kusambaza umeme, hivyo hakutakuwa na ugumu katika usambazaji umeme.

Dk Magufuli mwenye historia ya kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta ya barabara nchi nzima, alisema hayo jana kwenye mkutano wa kampeni, aliofanya mjini Bahi mkoani Dodoma. Kauli hiyo ya Dk Magufuli na nyingine ambazo amekuwa akitoa katika kampeni zake, zinazoingia katika mkoa wa Singida ambao ni wa 17 sasa, zimeonesha tofauti ya ahadi anazotoa kwa wananchi na zile zinazotolewa na mgombea wa urais wa Chadema, aliye chini ya mwamvuli wa Ukawa, Edward Lowassa. 

Tofauti kubwa imejionesha katika ahadi za Dk Magufuli, kwa kutambua na kuahidi kudumisha na kuendeleza kazi zilizofanywa na viongozi wa awamu zilizomtangulia na zinazoendelea kufanyika katika Awamu ya Nne inayoishia ukingoni.
Kwa upande wa Lowassa, yeye na wapigadebe wake wamekuwa wakionesha kwamba hakuna kilichofanyika katika miaka 54 iliyopita tangu nchi ilipopata Uhuru, wala kinachofanyika katika uongozi wa sasa.

Hata katika umeme, hawasemi kuwa kwa sasa Watanzania wanaopata nishati hiyo ni asilimia 46 kutoka asilimia 10 ya mwaka 2005, kutokana na jitihada za Serikali kwa kutumia fedha za ndani na nje, ambazo sasa zimeongezewa nguvu na fedha za MCC
Previous
Next Post »
Show Comments: OR

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com