Mchezaji wa Kimataifa wa Rugby Frans Malherbe wa South afrika amng'ata mchezaji wa Kimarekani uwanjani


Afrika ya kusini imekumbana na skendo mara ya pili na kudhaniwa labda ni ubaguzi wa rangi lakini haijathibitishwa hivyo. 

Hii imekuja baada ya ushaidi wa picha za video ambazo zilionyesha mchezaji huyo wa Afrika ya kusini akizamisha meno yake katika bega la mmarekani Matt Trouville na kumsababishia jeraha japo alikuwa amevaa kikinga mwili katika bega lake.

          Mchezaji Frans Malherbe akizamisha meno kwa Matt Trouville

Katika tukio hilo ambalo refalii Pascal Gauzere hakuweza kuliona kwa wakati huo linakuwa ni tukio la tatu kwa wachezaji wa kimataifa wa Afrika ya kusini kung'ata watu uwanjani.

      Frans Malherbe akiwa amemshika Matt Trouville kaika jaribio la kumn'gata

Mwaka 1994, Prop Johan Le Roux alimng'ata mnwizelandi hooker Sean Fitzpatrick’s sikio na akasimamishwa kwa muda wa mwaka mmoja na miezi sita (Miezi 18) baada ya vidhibitisho kukamilika.

Mwaka 1998, Kevin Yates alisimamishwa kwa muda wa miezi sita kwa kosa la umng'ata mchezaji mwenzie mwingereza Simon Fenn wakiwa uwanjani.

Kelvin Yates aliyefungiwa miezi sita baada ya kumng'ata Simon Fenn


Previous
Next Post »
Show Comments: OR

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com