Kamati ya maadili katika shirikisho
la soka duniani FIFA imependekeza Rais wa shirikisho la soka duniani
FIFA asimamishwe kazi kwa siku tisaini kwa tuhuma za Rushwa juu ya matumizi mabaya ya fedha za FIFA.
Wanachama wa kamati hiyo
walikutana wiki hii baada ya Jaji mkuu nchini Uswizi kufungua mashtaka
ya uhalifu dhidi ya Blatter mwezi uliopita.
Blatter anatuhumiwa
kwa kutia saini kandarasi zisizo na manufaa yoyote kwa FIFA mbali na
kufanya 'malipo' kwa rais wa shirikisho la UEFA Michel Platini.
Blatter
ambaye ni raia wa Uswizi amekuwa rais wa FIFA tangu mwaka 1998 na
Platini ambaye anataka kumrithi amekana madai yoyote ya kufanya uovu. Hakuna uamuzi ulioafikiwa kuhusu kumchukulia hatua yoyote Platini.
Chanzo: DailyMail
Sign up here with your email