UNDP yafadhili Kituo cha Mawasiliano cha NEC


TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imezindua kituo cha mawasiliano kusaidia wadau wa uchaguzi hasa wananchi na wapigakura kupata elimu ya mpigakura, kuuliza maswali kuhusu uchaguzi, pamoja na kulinda usalama.

Kwa kutumia kituo hicho kilichoko katika jengo la ofisi za NEC jijini Dar es Salaam, wapigakura watatumia namba ya simu 0800782100 kupiga bure na kuuliza maswali kuhusu uchaguzi mkuu, ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za kiusalama.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhani Kailima alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa kituo hicho kilichofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo (UNDP).

Alisema tangu Oktoba 12 hadi 18 mwaka huu, kituo kilianza kufanya kazi kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 12 jioni na kilimepokea maswali 444 na kutolewa ufafanuzi. Alisema kwa siku ya Jumanne pekee walipokea maswali 937 yanayohusu mwenendo wa uchaguzi, jinsi ya kupiga kura, kupotea kitambulisho na masuala mengine.

Alisema kuanzia Oktoba 19 hadi 30 mwaka huu, ndipo kituo kitafungwa kufanya kazi saa 24. Alisema wapo watendaji wa kutosha waliopata mafunzo maalumu kwa ajili ya kujibu na kutoa ufafanuzi wa masuala yote ya uchaguzi.

Kailima alisihi Watanzania kutotumia vibaya kituo hicho kwa kutoa lugha ya matusi au kufanya wengine kukosa mawasiliano, kwani wana mfumo maalumu kurekodi simu zote zinazotumika, zinazoingia au kufanya jambo lolote kinyume na kama lugha za matusi na kushtakiwa.

Akizungumzia upigaji kura, Kailima alisema kisheria hakuna mtu anayeweza kupiga kura katika kituo ambacho hakujiandikishia na kuwataka kutojisumbua kwenda kwani hawataruhusiwa.

Alisema sheria inasema wanaoruhusiwa kupiga kura sehemu yoyote ni mawakala, wagombea na watumishi wa tume, lakini kwa kujaza fomu maalumu na ikizingatiwa kama akipigia kata aliyojiandikisha, atapiga kura tatu.

“Lakini kama kata ni tofauti, atapiga ya mbunge na rais na kama jimbo ni tofauti na alipojiandikisha atapiga ya rais pekee huku wenye taarifa zenye utata kati ya Daftari la Wapigakura na kwenye kitambulisho nao watajaza fomu maalumu na kama hauna kadi hutaruhusiwa kupiga kura popote,” alisema.




Chanzo: Habari leo
Previous
Next Post »
Show Comments: OR

ConversionConversion EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com