KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel imezindua huduma nyingine ya
‘Yatosha’ itakayowezesha wateja wake kupiga simu Airtel kwenda Airtel na
kutuma ujumbe mfupi bila kikomo kwa kiwango cha Sh 300.
Aidha huduma hiyo pia inaambatana na kifurushi cha intaneti cha MB
10. Huduma hiyo inaitwa “Yatosha Nyts” inawawezesha wateja wa Airtel
nchi nzima kupiga simu Airtel kwenda Airtel na kutuma ujumbe mfupi
kwenda mitandao yote kila siku kuanzia saa 5:00 usiku hadi saa 12:00
asubuhi.
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Ofisa Uhusiano wa Airtel, Jane
Matinde alisema ‘Yatosha Nyts’ ni ofa kabambe na ya kipekee inayokidhi
mahitaji ya wateja wao. “Tumezindua “Yatosha Nyts” ofa kwa kuzingatia
mahitaji ya wateja wetu ya kuwasiliana na kupanga shughuli za siku
inayofuata bila hofu ya kupungukiwa na salio kwenye simu zao. “ alisema
Matinde.
Kujiunga na “Yatosha Nyts” mteja anatakiwa kupiga *149*99#.
Sign up here with your email
