Airtel Money kutoa gawio la bil.5.3/- kwa watumiaji wake.

Meneja Kitengo cha Airtel Money Asupya nalingigwa.

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel jana imetangaza kugawa zaidi ya Sh bilioni tano kwa wateja na mawakala wake wanaotumia huduma ya Airtel Money nchi nzima. Uamuzi huo wa kutoa gawio katika akaunti ya udhamini ya wateja wa Airtel Money litawawezesha wateja wa Airtel kulipwa kiwango kizuri cha gawio la faida.

Kiwango hiki cha pesa kitalipwa kutokana na kiasi cha pesa mteja alichokuwa nacho kwenye akaunti yake ya Airtel Money kila mwisho wa siku kuanzia Machi 2014 hadi Aprili 2015. Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa kitengo cha Airtel Money, Asupya Nalingigwa, alisema wanayo furaha kutangaza mgawanyo huo wa gawio la faida kwa wateja wao baada ya Benki Kuu ya Tanzania kuidhinisha kutoa pesa hizo katika akaunti ya udhamini ya pesa za wateja wa Airtel Money.

Alisema wateja wa Airtel Money watapata sehemu ya gawio lao kulingana na salio wanalokuwa nalo kwenye akaunti zao kila siku. Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma za kibunifu za kifedha kupitia simu za mkononi ikwemo NFC huduma inayokuwezesha kufanya malipo kupitia kadi, Mikopo ya Timiza na huduma nyingine nyingi.

Previous
Next Post »
Show Comments: OR

ConversionConversion EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com