![]() |
| Lupita Nyong'o |
NYOTA
wa filamu nchini Kenya
ambaye kwa sasa anaishi nchini Marekani, Lupita Nyong’o,
amesema wazazi wake wanamshawishi aolewe ili wapate wajukuu.
Lupita
kwa sasa anafanya vizuri katika filamu nchini Marekani na amefanikiwa kuchukua
tuzo za Oscar mapema mwaka huu, hivyo baada ya kupata tuzo hiyo alitembelea
nchini Kenya na kukutana na familia yake ambapo ilimtaka aolewe.
“Nilipokuwa
nchini Kenya wiki chache zilizopita nilikutana na familia yangu ambapo miaka
mingi tulikuwa hatujakutana, lakini mama yangu aliniambia kuwa huu ni muda wa
kutafuta mtoto hivyo natakiwa kuolewa.
“Lakini
kila kitu kina wakati wake, ninaamini muda ukifika nitaolewa na nitapata watoto
kama wazazi wangu wanavyotaka kuwa na wajukuu,” alisema Lupita.
Sign up here with your email
