Msafara wa Mgombea Urais wa CCM
Dkt Magufuli ukiwasili mjini Itigi mkoani Singida mapema jana mchana,tayari kwa
ajili ya kufanya mkutano wa kampeni mjini humo.
Mgombea
Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiombewa Dua na mmoja wa kiongozi wa dini
mara baada ya kusimamishwa na Wananchi wa kijiji cha Puma (hawapo pichani),
alipokuwa akielekea mkoani Singida mara baada ya kumaliza mkutano wake wa
hadhara wa kampeni.
Kiongozi
wa Msafara wa Kampeni za Mgombea Urais wa CCM Dkt John Magufuli,Ndugu Abdallah
Bulembo akimkaribisha Mgombea Urais wa CCM Dkt.Magufuli kuwahutubia wananchi wa
Ikungi jioni ya jana na kuwaomba kumpigia kura ya ndio ifikapo Oktoba 25 mwaka
huu kwenye uchahuzi mkuu wa Urais,Wabunge na Madiwani.
Mgombea wa urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia
wananchi kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mnadani
Ikungi mkoani Singida jioni ya jana ,wakati akiwaomba wananchi hao
kumpigia kura za ndiyo ifikapo Oktoba 25 mwaka huu katika uchaguzi wa Rais ,
Wabunge na Madiwani.
Dkt. Magufuli amesema serikali yake
itahakikisha inazisaidia taasisi mbalimbali hasa za mashirika ya
dini ambazo zinaendesha hospitali katika kupata vifaa, Ruzuku, na
ajira kwa wafanyakazi ili kuimarisha huduma za kiafya kwa jamii.
Wananchi wakiwa wamekusanyika
kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mnadani Ikungi mkoani
Singida,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli aliwahutubia na pia
kuwaomba wananchi hao kumpigia kura za ndiyo ifikapo Oktoba 25 mwaka huu
katika uchaguzi wa Rais , Wabunge na Madiwani.
Sign up here with your email



