John Pombe Pombe Joseph Magufuli
Mgombea urais kupita CCM kitaaluma ni Mwalimu na mtalaamu wa Kemia
aliyezaliwa October 29 mwaka 1959 huko Chato mkoani Kagera Kaskazini
magharibi mwa Tanzania.
Alipata elimu ya msingi katika shule ya
msingi huko huko Chato, mkoani Kagera kati ya mwaka 1967 hadi 1975 na
baadae kujiunga na chuo cha ualimu Mkwawa kilichopo Iringa kusini
mashariki mwa Tanzania kati ya mwaka 1979 na 1982 ambapo alitunukiwa
Stahahada ya Ualimu na kuanza kufundisha masomo ya hisabati na kemia
katika shule mbali mbali za sekondari kuanzia mwaka 1983.
John
Pombe Magufuli hakuishia hapo kielemu kwani aliamua kujendeleza zaidi
ambapo alijiunga na chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1985 hadi 1988
ambapo na kutunikiwa shahada ya ualimu katika masomo ya chemia na
hisabati ambapo baadae alijikita zaidi katika somo la Kemia kusomea hadi
nganzi ya udaktari.
Katika siasa za Tanzania John Pombe Magufuli
mwanzoni hakujulikana sana, hadi nyota yake ya kisiasa ilianza kung'aa
pale alipogombea na kushinda ubunge mwaka 1995 ambapo mwaka huo huo
aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wizara ya Ujenzi na baadae kupanda ngazi
hadi kuwa waziri kamili nafasi aliyonayo hadi hivi sasa.
Wasifu wa
nje ya Mshika bendera huyo wa chama cha Mapinduzi CCM katika ngazi ya
urais kwa mujibu wa majirani wanaoishi karibu na nyumba yake jijini Dar
es Salaam wasema ni anaishi maisha ya kawaida kwani wakati watoto wa
baadhi ya viongozi wakisoma shule za hali ya juu watoto wake wamesoma
katika shule za kawaida.
Kwa sasa Dr. John Pombe Joseph Magufuli
ndiye mshika bendera ya urais kupitia chama tawala. Hata hivyo tofauti
na uchaguzi uliopita mgombea huyo anakabiliwa na upinzani mkali kutoka
kwa mgombea wa upinzani Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hii Edward Lowassa
ambaye anagombea kupitia chama cha upinzani cha CHADEMA akiwakilisha
muungano usio rasmi wa vyama vinne vya upinzani unaojulikana UKAWA.
Chanzo: BBC Swahili
Sign up here with your email