WASIFU: Mfahamu Dokta Ali Mohamed Shein


Zimesalia siku takriban 19 kabla ya Watanzania kupiga kura kwenye uchanguzi mkuu utakaofanyika October 25 mwaka huu.
 
Dokta Ali Mohammed Shein ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya Urais katika serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,anatarajia kutetea kiti chake na kumaliza muhula wa pili wa uongozi wake, kwa mujibu wa sheria.
Dokta Ali Mohamed Shein alizaliwa machi 13, 1948. Amehitimu katika fani ya Biokemia ya Utabibu kutoka Chuo kikuu cha Odessa nchini Urusi na pia kupata elimu zaidi Uingereza.

Waswahili wanasema nyota njema honekana asubuhi, kwa dokta Shein umahiri wake katika uongozi ulianza kuonekana bado akiwa kijana mdogo, kwani mbali na mbio zake kisiasa kuanza pale alipojiunga na Umoja wa Vijana wa chama cha Afro-Shirazi wakati akiwa shule, pia alikuwa na kipaji kingine cha uongozi, katika sekta ya michezo.

Dokta Mohammed Saleh Jidawy ni Katibu mkuu Wizara ya Afya Zanzibar na alisoma na dokta Shein katika shule ya Lumumba, Unguja.
Anasema enzi zake, Dr Shein alikuwa mwanariadhaa hodari mpaka kuwa nahodha katika timu ya shule ya riadha.


Harakati zake kisiasa zinaonekana kuanzia wakati wa ujana wake,ambapo vijana wengi wa kiafrika walikosa nafasi ya kupata elimu, na katika misingi hiyo alianza shughuli zake za kijamii, kwa kushiriki pia kutoa elimu kuwezesha vijana kujielewa, hususan kielimu na kujiandaa kisiasa kupitia chama chake cha siasa cha Afro Shiraz.
 
Kutokana na nafasi hiyo aliteuliwa kwenye Kamati Kuu ya CCM 2005.
Alishinda Kiti cha Uwakilishi cha Mkanyageni katika uchaguzi mkuu wa Novemba 6, 2000 na kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Aliteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba na Utawala Bora, Novemba 22, 2000.


Nafasi ambayo pengine ilifungua njia zaidi kwa yeye kupanda juu kiuongozi
Kisiasa zaidi alifahamika Julai 13, mwaka 2001, wakati Dokta Shein alipoteuliwa kuwa makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kufanya kazi pamoja na Rais wa wakati huo Benjamin Mkapa.

Annet Mtawali Ngahyoma ni mmoja ya waliobahatika kufanya kazi na Dokta Shein mara tu alipoteuliwa kuwa Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anamuelezea kuwa ni mpole na mwenye kupenda dini.



Katika Uchaguzi Mkuu wa 2005, Dokta Mohammed Shein aliteuliwa kuwa mgombea mweza kupitia Chama cha Mapinduzi, Na hatimaye kuwa Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuapishwa 21 Desemba, 2005, baada ya CCM kuendelea kuongoza nchi.

Kwa mara ya kwanza aligombea nafasi ya Rais wa Zanzibar katika Uchaguzi mkuu wa Oktoba 31 mwaka 2010 na kushinda, hivyo kuapishwa kuwa rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Novemba 3 mwaka 2010.

Dokta Shein ni mtu mwenye msimamo asiyeyumbishwa katika kile anachokiamini, na hata kuonekana kiongozi imara aliyeweza kuongoza serikali ya Umoja wa Kitaifa, bila ya kuterereka licha ya shutuma alizotupiwa toka pande zote.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2015, Dokta ali Mohamed Shein anawania tena kiti hicho ikiwa ni muhula wa pili na wa mwisho kwa mujibu wa sheria.
Previous
Next Post »
Show Comments: OR

ConversionConversion EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng

Contact us

Name

Email *

Message *

Tangaza nasi

Tangaza nasi
Freebango.com